Wangoi wote malenga, watunzi wa kila fani
Naja nikipiga benga, ingawa nina huzuni
Leyo nyama naifunga, n'ole ata'yebaini
Hini ni kalamu gani, utakacho yaandika?
Ina nembo almasi, uchunguzapo makini
Ndaniye wino wa ngisi, haufutiki jamani
Yatumiwa na wakwasi, haifai masikini
Hini ni kalamu gani, utakacho yaandika?
Ukitaka rithi mke, uitowe mfukoni
Kisha nayo uandike, atakuja kiamboni
Lakini ubaya wake, kwa mke penzi huoni!
Hini ni kalamu gani, utakacho yaandika?
Ukihitaji mavazi, na mapambo muilini
Ujipake hina ngozi, waja wakakutamani
Bali sura h'igeuzi, kama u nyani u nyani
Hini ni kalamu gani, utakacho yaandika?
Utakacho itakupa, bali ina walakini!
Watu watakuogopa, 'kiwa nayo mkononi
Bali utatapatapa, kukosa utu insani
Hini ni kalamu gani, utakacho yaandika?
'Kiwa nayo husumbuki, licha zake nukusani
'Tapita kwenye bunduki, mitutu ya kila kani
Bali hayondoi chuki, kati yako na wendani
Hini ni kalamu gani, utakacho yaandika
Huu ndio mtandao wa kipekee utakaowaauni wapenzi na wakereketwa wa lugha ya Kiswahili. Nimeubuni ili kukuza kipawa, usanii na utamaduni. Utaasika, udadisi na licha ya kuelimika, utaburudika. Usikose kuniachia ujumbe wako, ili nami nijielewe. Asante na karibu.
Ijumaa, 12 Aprili 2019
NITANENA
Kamwe sikomi kunena, maneno yenye maana
Nitanena kwa kudona, vimbwenga vinotubana
Nisiponena natuna, na moyo kujaa suna
Nitanena nikapona, kazi mbi ninaikana!
Nitayanena kwa kina, niuondowe uguna
Ninene mambo bayana, yanounga uungwana
Japo mtanitukana, nitukane kutukana
Nitanena nikapona, nyendo mbi nimezikana!
Sinyamazi nitanena, mdomo hujashikana
Msipotaka ninena, njoni kinywa mnishona
Ama mkatangamana, ili kushirikiana
Nitanena nikapona, ukabila naukana!
Maneno yana amana, walimu kwenda kwa wana
Hushauri kupatana, washari wakikinzana
Neno huleta fitina, na kwalo suluhu kuna
Nitanena nikapona, tuacheni kugombana!
Nitanena tena sana, ninene neno anana
Kwamba tuna kuungana, umoja na kupendana
Kwa marefu na mapana, tuisome Qur'ana
Nitanena nikapona, Biblia imenena!
Ugomvi, ushirikina, wizi, kuto'miniana
Ufisadi naukana, na ubakaji vimwana
Ujambazi hufishana, huleta ukata tena
Nitanena nikapona, nimepona nimena!
Nitanena kwa kudona, vimbwenga vinotubana
Nisiponena natuna, na moyo kujaa suna
Nitanena nikapona, kazi mbi ninaikana!
Nitayanena kwa kina, niuondowe uguna
Ninene mambo bayana, yanounga uungwana
Japo mtanitukana, nitukane kutukana
Nitanena nikapona, nyendo mbi nimezikana!
Sinyamazi nitanena, mdomo hujashikana
Msipotaka ninena, njoni kinywa mnishona
Ama mkatangamana, ili kushirikiana
Nitanena nikapona, ukabila naukana!
Maneno yana amana, walimu kwenda kwa wana
Hushauri kupatana, washari wakikinzana
Neno huleta fitina, na kwalo suluhu kuna
Nitanena nikapona, tuacheni kugombana!
Nitanena tena sana, ninene neno anana
Kwamba tuna kuungana, umoja na kupendana
Kwa marefu na mapana, tuisome Qur'ana
Nitanena nikapona, Biblia imenena!
Ugomvi, ushirikina, wizi, kuto'miniana
Ufisadi naukana, na ubakaji vimwana
Ujambazi hufishana, huleta ukata tena
Nitanena nikapona, nimepona nimena!
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)