Ningekuwa na mabawa, kama ndege ningeruka
Nifike kwenye maziwa, penye misitu na nyika
Kumshukuru Moliwa, aloniongeza mwaka
Mwakani naikumbuka, siku niliyozaliwa!
Shaabani ilikuwa, themanya-sidusi mwaka
Ishirini-tatu chwewa, mapema kupambazuka
Fatiha ikajibiwa, myezi kenda kutimika
Mwakani naikumbuka, siku niliyozaliwa!
Nisaidieni njiwa, makero kutambilika
Swala njema kuombewa, kwa khatwiri ya shufaka
Mema piya kutakiwa, nyoyonimwe wahibaka
Mwakani naikumbuka, siku niliyozaliwa!
Vinono nikichinjiwa, siwezi nikaridhika
Dengeluwa kujaziwa, na keki za kubanika
Nishirikishie duwa, kwa Mola na malaika!
Mwakani naikumbuka siku niliyozaliwa!
SHEREHE ZA KUADHIMISHA MWAKA WANGU WA 25.
KWA WAPENZI WANGU WOTE WENYE NIA NJEMA NA DHAMIRI.
Huu ndio mtandao wa kipekee utakaowaauni wapenzi na wakereketwa wa lugha ya Kiswahili. Nimeubuni ili kukuza kipawa, usanii na utamaduni. Utaasika, udadisi na licha ya kuelimika, utaburudika. Usikose kuniachia ujumbe wako, ili nami nijielewe. Asante na karibu.
Jumatano, 21 Agosti 2013
HONGERA KISURA!
Nema naja jukwaani, kuikatisha subira!
Niseme yalo moyoni, tuloshushiwa ghufira
Nipokeze shuqrani, shule'etu kutia fora!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Wahitaji shuqrani, Tabitha wetu kisura
Matokeo ya mwakani, tukapata kumi bora
Siwavalii miwani, walimu wetu hongera!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Ulotenda mhisani, shuleni siyo hasara
Mikataba kusaini, vitabu tukavidara
Kapita madarasani, ukapeana busara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Makelele vidatoni, walokuwa kuzurura
Walopoteza imani, wote kawapa tijara
Akaziweka kanuni, zikasimama imara!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Makelele vidatoni, walokuwa kuzurura
Walopoteza imani, wote kawapa tijara
Akaziweka kanuni, zikasimama imara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Toka juu hadi chini, aliunganisha dira
Walimu wa afisini, wakatuvunjia nira
Tukaingia vitani, tukaacha masihara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Wazazi waliamini, wakavaa matambara
Mwana aende shuleni, kujiundia ijara
Leo tupo shereheni, wazazi wetu hongera!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Vitabu maktabani, na kujengwa maabara
Ni mwanzo wa tumaini, kujaliwa madhukura
Tuingie masomoni, tuitimize ishara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Asante wetu wageni, mumetujaza fikara
Kupita ni letu deni, nawaombea subira
Sikusahau Diwani, Bibao George Morara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Wanafunzi jikazeni, msije mkatukera
Muingie vyuoni, tufukuze ufukara!
Kerongorori jamani, siku zote tukang'ara!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Malenga wa Msituni, niwapokeze taswira
Mwaka huu hamsini, watafata taashira
Mola utupe hisani, tufyatuke ja kombora!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
KWA MWALIMU MKUU,
BI. TABITHA MOGONCHI,
SHULE YA MSETO, KUTWA NA MALAZI - UPILI, KERONGORORI.
(Shairi hili, nililitunga na kulighani nikiwa mwanafunzi kidato cha nne, katika sherehe SIKUKUU YA TUZO, Mei 15, 2009).
Niseme yalo moyoni, tuloshushiwa ghufira
Nipokeze shuqrani, shule'etu kutia fora!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Wahitaji shuqrani, Tabitha wetu kisura
Matokeo ya mwakani, tukapata kumi bora
Siwavalii miwani, walimu wetu hongera!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Ulotenda mhisani, shuleni siyo hasara
Mikataba kusaini, vitabu tukavidara
Kapita madarasani, ukapeana busara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Makelele vidatoni, walokuwa kuzurura
Walopoteza imani, wote kawapa tijara
Akaziweka kanuni, zikasimama imara!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Makelele vidatoni, walokuwa kuzurura
Walopoteza imani, wote kawapa tijara
Akaziweka kanuni, zikasimama imara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Toka juu hadi chini, aliunganisha dira
Walimu wa afisini, wakatuvunjia nira
Tukaingia vitani, tukaacha masihara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Wazazi waliamini, wakavaa matambara
Mwana aende shuleni, kujiundia ijara
Leo tupo shereheni, wazazi wetu hongera!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Vitabu maktabani, na kujengwa maabara
Ni mwanzo wa tumaini, kujaliwa madhukura
Tuingie masomoni, tuitimize ishara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Asante wetu wageni, mumetujaza fikara
Kupita ni letu deni, nawaombea subira
Sikusahau Diwani, Bibao George Morara
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Wanafunzi jikazeni, msije mkatukera
Muingie vyuoni, tufukuze ufukara!
Kerongorori jamani, siku zote tukang'ara!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
Malenga wa Msituni, niwapokeze taswira
Mwaka huu hamsini, watafata taashira
Mola utupe hisani, tufyatuke ja kombora!
Bibi Tabitha hongera, uongoze shule yetu!
KWA MWALIMU MKUU,
BI. TABITHA MOGONCHI,
SHULE YA MSETO, KUTWA NA MALAZI - UPILI, KERONGORORI.
(Shairi hili, nililitunga na kulighani nikiwa mwanafunzi kidato cha nne, katika sherehe SIKUKUU YA TUZO, Mei 15, 2009).
KAZI YANGU (MAHASIDI)
Kazi yangu ya mikono, ndugu nishapowambia
Ni mshipi wa kiuno, nitakapojifungia
Mbona yenu minong'ono, pote mnapotembea?
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Finyango nazofinyanga, Mola amenijalia
Mbona msipojitenga, matusi mwanitupia?
Kwa nini mnanipinga, mwanisengenyea pia?
Mbona mnajisumbua nifanyapo kazi yangu?
Wema tenda zako nenda, wahenga walitwambia
Yenu mnayoyatenda, ni nani mtagaia?
Kazi yangu nayopenda, mbali mwaitupilia!
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Kama mngekuwa wema, auni kunichangia
Mnipe busara njema, nami ningewaungia
Sasa mwaipanga njama, mwataka kuniulia!
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Mmenisumbua sana, mori imenipandia
Sipendi kufarakana, na watu wasio njia
Mwajifanya mnaona, hamnazo kujitia
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Kaditama wa tamati, utunzi kumalizia
Hela nenda jizatiti, kazi zenu jifanyia
Naitwa Nema Sereti, ujumbe nawatilia
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
DIWANI YA "UREMBO WA NEMA, 2003".
Ni mshipi wa kiuno, nitakapojifungia
Mbona yenu minong'ono, pote mnapotembea?
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Finyango nazofinyanga, Mola amenijalia
Mbona msipojitenga, matusi mwanitupia?
Kwa nini mnanipinga, mwanisengenyea pia?
Mbona mnajisumbua nifanyapo kazi yangu?
Wema tenda zako nenda, wahenga walitwambia
Yenu mnayoyatenda, ni nani mtagaia?
Kazi yangu nayopenda, mbali mwaitupilia!
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Kama mngekuwa wema, auni kunichangia
Mnipe busara njema, nami ningewaungia
Sasa mwaipanga njama, mwataka kuniulia!
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Mmenisumbua sana, mori imenipandia
Sipendi kufarakana, na watu wasio njia
Mwajifanya mnaona, hamnazo kujitia
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
Kaditama wa tamati, utunzi kumalizia
Hela nenda jizatiti, kazi zenu jifanyia
Naitwa Nema Sereti, ujumbe nawatilia
Mbona mnajisumbua, nifanyapo kazi yangu?
DIWANI YA "UREMBO WA NEMA, 2003".
MPENZI, NAKUPA MOYO
Wapo wanaotafuta, wa kumpenda hawana!
Wewe ndiwe nilipata, maishani kupendana
Ashiya wa bukhrata, hatima ya kukutana
Ingawaje mali sina, mpenzi, nakupa moyo.
Usiyependa maringo, majigambo wewe huna
Umbole la mviringo, alilokupa Rabana
Una ya upanga shingo, nywele zilizojichana
Mrembo wangu Regina, mpenzi, nakupa moyo!
Sura yako afya kwako, hata ujipake hina
Roho ya mtu iliko, ndiko kwenyeye hazina!
Nema nimetuwa kwako, azizi Wango Regina
Nitakachokupa Nana, Mpenzi, nakupa moyo!
Kila mara nakuwaza, usiku hata mchana
Ndiwe ninayetukuza, bila wewe raha sina
Usije kunipuuza, mpenzi sinitukana!
Kusudi kutulizana, Mpenzi, Nakupa moyo!
Kila mara nakuwaza usiku hata mchana
Ndiwe ninayetukuza, bila wewe raha sina
Usije kunipuuza, mpenzi sinitukana!
Kusudi kutulizana, Mpenzi, Nakupa moyo!
Wango kito cha thamani, ni wewe mwengine sina
Nipe raha maishani, tuishi tukipendana
U malaika wa shani, huna wa kumfanana!
Umenipendeza sana, Mpenzi, Nakupa moyo!
Mwisho nanga naitia, kukuimbia Regina
Leo nakufichulia, Nema nakupenda sana!
Tuhifadhi yetu ndoa, Mola akatupe wana!
Mimi nawe twatoshana, Mpenzi, Nakupa moyo!
KWA MKE WANGU MPENDWA,
REGINA WANGO NEMA,
"KUMBUKUMBU ZA NDOA YETU - MIAKA MIWILI"
Julai 17, 2012.
Wewe ndiwe nilipata, maishani kupendana
Ashiya wa bukhrata, hatima ya kukutana
Ingawaje mali sina, mpenzi, nakupa moyo.
Usiyependa maringo, majigambo wewe huna
Umbole la mviringo, alilokupa Rabana
Una ya upanga shingo, nywele zilizojichana
Mrembo wangu Regina, mpenzi, nakupa moyo!
Sura yako afya kwako, hata ujipake hina
Roho ya mtu iliko, ndiko kwenyeye hazina!
Nema nimetuwa kwako, azizi Wango Regina
Nitakachokupa Nana, Mpenzi, nakupa moyo!
Kila mara nakuwaza, usiku hata mchana
Ndiwe ninayetukuza, bila wewe raha sina
Usije kunipuuza, mpenzi sinitukana!
Kusudi kutulizana, Mpenzi, Nakupa moyo!
Kila mara nakuwaza usiku hata mchana
Ndiwe ninayetukuza, bila wewe raha sina
Usije kunipuuza, mpenzi sinitukana!
Kusudi kutulizana, Mpenzi, Nakupa moyo!
Wango kito cha thamani, ni wewe mwengine sina
Nipe raha maishani, tuishi tukipendana
U malaika wa shani, huna wa kumfanana!
Umenipendeza sana, Mpenzi, Nakupa moyo!
Mwisho nanga naitia, kukuimbia Regina
Leo nakufichulia, Nema nakupenda sana!
Tuhifadhi yetu ndoa, Mola akatupe wana!
Mimi nawe twatoshana, Mpenzi, Nakupa moyo!
KWA MKE WANGU MPENDWA,
REGINA WANGO NEMA,
"KUMBUKUMBU ZA NDOA YETU - MIAKA MIWILI"
Julai 17, 2012.
Jumatano, 14 Agosti 2013
NARUDI KWETU NARUDI
Nimechoka tangatanga, kila tengo nimefika!
Mithili mtu mjinga, vizuri asojiweka!
Yamenifinya majanga, utumwani kuteseka!
Kurudi kwetu nataka, duniya imenisonga!!!
Duniya imenisonga, kurudi kwetu nataka!
Kwa nini nilijitenga, na watu walosifika?
Kwangu huku kutochunga, kumenileta mashaka!
Kurudi kwetu nataka, nimekonda sina hali!!!
Nimekonda sina hali, kurudi kwetu nataka!
Hata usiku silali, naumu zimen'toweka!
Mavazi sina sijali, kufa nani anataka?
Kurudi kwetu nataka, nani atanikubali?
Nani atanikubali, kurudi kwetu nataka!
Chawa wamenikabili, damu yangu waitaka!
Kila mtu hanijali, viumbe vyanitoroka!
Kurudi kwetu nataka, ugenini kuna dhiki!
Kweli nimeisha hamu, narudi kwetu nyumbani!
Yamenichusha magumu, nilopata ugenini!
Nusura nife Kisumu, kwa maradhi kitandani!
Hata kama pawe duni, nyumbani kweli patamu!
Ola nilivoduwaa, sina wa kuniauni!
Hata nikiwa kazini, kamwe sikufurahia
Hata hivyo kazi gani, pato wanakukatia?
Sitaki kufanya deni, nianze kufatilia!
Nyumbani ni nyumbani tu, hata kama ni chooni!
Siku nzima shinda njaa, pesa huna mfukoni!
Hata nikawe shujaa, magonjwa yapigwe nini?
Narudi kwetu nyumbani, ugeni sitakaa!
DIWANI YA MRATIBU, 2013.
Mithili mtu mjinga, vizuri asojiweka!
Yamenifinya majanga, utumwani kuteseka!
Kurudi kwetu nataka, duniya imenisonga!!!
Duniya imenisonga, kurudi kwetu nataka!
Kwa nini nilijitenga, na watu walosifika?
Kwangu huku kutochunga, kumenileta mashaka!
Kurudi kwetu nataka, nimekonda sina hali!!!
Nimekonda sina hali, kurudi kwetu nataka!
Hata usiku silali, naumu zimen'toweka!
Mavazi sina sijali, kufa nani anataka?
Kurudi kwetu nataka, nani atanikubali?
Nani atanikubali, kurudi kwetu nataka!
Chawa wamenikabili, damu yangu waitaka!
Kila mtu hanijali, viumbe vyanitoroka!
Kurudi kwetu nataka, ugenini kuna dhiki!
Kweli nimeisha hamu, narudi kwetu nyumbani!
Yamenichusha magumu, nilopata ugenini!
Nusura nife Kisumu, kwa maradhi kitandani!
Hata kama pawe duni, nyumbani kweli patamu!
Ola nilivoduwaa, sina wa kuniauni!
Hata nikiwa kazini, kamwe sikufurahia
Hata hivyo kazi gani, pato wanakukatia?
Sitaki kufanya deni, nianze kufatilia!
Nyumbani ni nyumbani tu, hata kama ni chooni!
Siku nzima shinda njaa, pesa huna mfukoni!
Hata nikawe shujaa, magonjwa yapigwe nini?
Narudi kwetu nyumbani, ugeni sitakaa!
DIWANI YA MRATIBU, 2013.
GUGUMAJI (IBILISI MREMBO)
Ziwani linabishana, na samaki ufukweni!
Kwa kasi kuzaliana, bali halina thamani!
Sura huvutia sana, ndani maficho ya jini!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
Limenitenda kichuna, zogo na purukushani
Usiku hata mchana, sina furaha moyoni
Kufyeka na kuvutana, tabia za kishetani!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
Juu maji 'kiliona, ni uwanja wa kijani
Chini maji yajazana, kukuhadaa machoni!
Vijinyama vimechina, kukosa okisijeni!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
Kwa urembo limefana, bali vitendo ni duni!
Kwanza nilipoliona, nilihisi burudani!
Bali uhai halina, lafisha kama tufani!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
Mmea huu mpana, na mingine hufanani!
Kwenye maji hapa mbona, unapataje madini?
Siutaki naukana, wavuvi tu vilioni!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
Wataishi vipi ngwena, na samaki mashakani?
Nasi ndo yetu hazina, kwa wenyeji na wageni
Madau, meli, safina, hazipiti abadani!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
Nani atapatikana, asiliye abaini?
Gugumaji kulichuna, viumbe kuviauni
Nema kichwa najikuna, nirudipo Msituni!
Nimepata nilidhani, kumbe nimepatikana!
DIWANI YA "MRATIBU", 2013.
Jumapili, 11 Agosti 2013
NYOTA YANGU
Nyota yangu ya thamani, nahitaji kukuona
Umenikaa moyoni, bila wewe sitapona
Wapotelea gizani, ninapolala kichuna!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Nimeshindwa kutulia, na imenikumba suna
Usiku kukungojea, nguvu za kukesha sina!
Ghafula ninasinzia, kwa usingizi wa kina
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Mchana nina nafasi, mie nawe kuonana!
Tujilaze kwenye nyasi, ya moyoni kuyanena
Twondowane wasiwasi, mawazo kutulizana!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Mwangaza wako wa shani, wanijaza uchu sana!
Ndio ninaotamani, kwenye anga la mchana
Nakuomba niauni, nyota yangu ya maana!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Giza linapoingia, wenzi wananitukana
Shere wananifanyia, ndoto yangu kuibana
Bali nitavumilia, madhali tunapendana!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Kigae cha almasi, uso uliojipuna
Nakomea hapa basi, nimejua hutanuna!
Ushindane na shamsi, usiku ung'ae tena!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Umenikaa moyoni, bila wewe sitapona
Wapotelea gizani, ninapolala kichuna!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Nimeshindwa kutulia, na imenikumba suna
Usiku kukungojea, nguvu za kukesha sina!
Ghafula ninasinzia, kwa usingizi wa kina
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Mchana nina nafasi, mie nawe kuonana!
Tujilaze kwenye nyasi, ya moyoni kuyanena
Twondowane wasiwasi, mawazo kutulizana!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Mwangaza wako wa shani, wanijaza uchu sana!
Ndio ninaotamani, kwenye anga la mchana
Nakuomba niauni, nyota yangu ya maana!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Giza linapoingia, wenzi wananitukana
Shere wananifanyia, ndoto yangu kuibana
Bali nitavumilia, madhali tunapendana!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
Kigae cha almasi, uso uliojipuna
Nakomea hapa basi, nimejua hutanuna!
Ushindane na shamsi, usiku ung'ae tena!
Nyota yangu ya usiku, nakutamani mchana!
BIN-ADAM
Nina kauli-kinzani, peupe naianika!
Ituhusuyo insani, na sifa tunojivika
Majigambo midomoni, mwenzi-kwa-mwenzi mipaka!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Tajiri na masikini, wapi wote walitoka?
Kujigamba na mapeni, jumba, gari, madaraka!
Mkata mwenye huzuni, isitoshe wamcheka!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Nayaingilia ndani, naomba kueleweka!
Unapoenda bafuni, kukoga ukasafika
Wapangusa maungoni, na marashi kujipaka
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Urembo wako mwilini, aliokupa Rabuka
Unakufanya huoni, wengine ni takataka!
Usifanye uhaini, mawaidha kutapika
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Ningeishi mawinguni, ningekuwa malaika!
Kuliko ulimwenguni, huku kulikochafuka!
Mtu ni utu jamani, bure unachacharika!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Towa nta sikioni, binadamu msifika
Alotuumba Manani, duniani katuweka
Pua zyangalie chini, na ndipo tulipotoka
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Nenda zangu Msituni, nikiwa nimeudhika
Bali furaha moyoni, kwa ujumbe kunitoka!
Sote tujivishe soni, ja nguo zimeraruka!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Ituhusuyo insani, na sifa tunojivika
Majigambo midomoni, mwenzi-kwa-mwenzi mipaka!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Tajiri na masikini, wapi wote walitoka?
Kujigamba na mapeni, jumba, gari, madaraka!
Mkata mwenye huzuni, isitoshe wamcheka!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Nayaingilia ndani, naomba kueleweka!
Unapoenda bafuni, kukoga ukasafika
Wapangusa maungoni, na marashi kujipaka
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Urembo wako mwilini, aliokupa Rabuka
Unakufanya huoni, wengine ni takataka!
Usifanye uhaini, mawaidha kutapika
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Ningeishi mawinguni, ningekuwa malaika!
Kuliko ulimwenguni, huku kulikochafuka!
Mtu ni utu jamani, bure unachacharika!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Towa nta sikioni, binadamu msifika
Alotuumba Manani, duniani katuweka
Pua zyangalie chini, na ndipo tulipotoka
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
Nenda zangu Msituni, nikiwa nimeudhika
Bali furaha moyoni, kwa ujumbe kunitoka!
Sote tujivishe soni, ja nguo zimeraruka!
Kama u safi, taulo, inachafuka kwa nini?
SILI NYAMA YA NGURUWE!
Sili nyama ya nguruwe, leo nimeitambua!
Nimeikana mwenyewe, bila mtu kunambia!
Inanitia kiwewe, pia inanichafua!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Silazii nipikiwe, mboga zijapokosea
Hamu isinizuzuwe, zama nikikumbukia
Muwele sitaki niwe, nilokula yatoshea!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Nilisoma nimwelewe, kwa nini twamchukia!
Mola hataki aliwe, Qur'ani na Biblia
Mbali akatupiliwe, alipo kupakimbia!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Wacha mbwa wapikiwe, wao watafurahia!
Sitaki nipambaniwe, Jehannam n'kaingia
Na kwangu asifugiwe, sina chembe ya hisia
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Harufu yake nguruwe, pote anapopitia
Ataka mumtambuwe, msipomuangalia
Ni benibeni mwendowe, tapishi kwake halua!
Ni nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Ni vyema nikashifiwe, na wenzangu familia
Wala cheo nisipewe, kundi kulisimamia!
Bali kufuga nguruwe, nimekana niachia!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Kwa mafuta asifiwe, na juhudi kitabia
Kila kitu akijuwe, anuse na kujilia
Atamani mbele awe, kwanza mapya kupokea!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Watalii wachinjiwe, uchu kuwaondolea!
Filamu wachukuliwe, wa ng'ambo kupelekea!
Ama mbwa wapikiwe, na punda kufurahia!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Kitambo niing'wafuwe, sikuwa nimeijua!
Sasa leo iepuwe, ni haramu nisikia!
Mara ngapi muambiwe, kwamba ni mbaya! Yaua!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Yanipa maruweruwe, ijazwapo sufuria!
Nashindwa vipi iliwe, na mbwa waingojea!
Ninakoma nipumuwe, ujumbe huu pokea:
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Nimeikana mwenyewe, bila mtu kunambia!
Inanitia kiwewe, pia inanichafua!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Silazii nipikiwe, mboga zijapokosea
Hamu isinizuzuwe, zama nikikumbukia
Muwele sitaki niwe, nilokula yatoshea!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Nilisoma nimwelewe, kwa nini twamchukia!
Mola hataki aliwe, Qur'ani na Biblia
Mbali akatupiliwe, alipo kupakimbia!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Wacha mbwa wapikiwe, wao watafurahia!
Sitaki nipambaniwe, Jehannam n'kaingia
Na kwangu asifugiwe, sina chembe ya hisia
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Harufu yake nguruwe, pote anapopitia
Ataka mumtambuwe, msipomuangalia
Ni benibeni mwendowe, tapishi kwake halua!
Ni nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Ni vyema nikashifiwe, na wenzangu familia
Wala cheo nisipewe, kundi kulisimamia!
Bali kufuga nguruwe, nimekana niachia!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Kwa mafuta asifiwe, na juhudi kitabia
Kila kitu akijuwe, anuse na kujilia
Atamani mbele awe, kwanza mapya kupokea!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Watalii wachinjiwe, uchu kuwaondolea!
Filamu wachukuliwe, wa ng'ambo kupelekea!
Ama mbwa wapikiwe, na punda kufurahia!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Kitambo niing'wafuwe, sikuwa nimeijua!
Sasa leo iepuwe, ni haramu nisikia!
Mara ngapi muambiwe, kwamba ni mbaya! Yaua!
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
Yanipa maruweruwe, ijazwapo sufuria!
Nashindwa vipi iliwe, na mbwa waingojea!
Ninakoma nipumuwe, ujumbe huu pokea:
Ni 'nyama mwenye udhia, sili nyama ya nguruwe!
JERAHA LA MOYO
Moyoni nimeumiya, nimepagazwa kupenda
Juhudi nilizotiya, tiarangu kuiunda
Hewani kuitezeya, na upepo ikaenda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Angani ilipo'ngiya, eneole ikatanda
Uzi nikaachiliya, 'kadhani itajipinda
Nyuma kuifatiliya, tiara 'kazidi kwenda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Wapi imepoteleya, tiara niliyopenda?
Vipi nitaifikiya, na kupaa kwanishinda?
Ni hofu kuvumiliya, na jinsi nilivyokonda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Mlo nazo 'sinambiya, nimeapa kutopenda!
Tiara zina kayaya, kupozi nazo kwa inda!
H'wenda ikawa kinaya, dhidi ya pepo 'zilinda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Ahsante sana hewala, kwa auni za busara!
Nilikuwa nimelala, nikiwaza kwa hasira
Bali nasema Inshalla! Nitaipata tijara!
Nilomsifu "Tiara", kwangu ameshakugura!
Pishi nashindwa kulila, pendo halina sitara
Chumba tulopamba sala, nakiona ja ahera
Mola ukiwa ni hila, nipe mwengine kisura!
Nilomsifu "Tiara", kwangu ameshakugura!
Nimelingana kwa Mola, atujeze maghufira
Apate alo aula, nami nimpate bora
Mambo yasiwe ghafula, huvuta heri subira!
Nilomsifu "Tiara", kwangu ameshakugura!
DIWANI YA MRATIBU, 2013.
Juhudi nilizotiya, tiarangu kuiunda
Hewani kuitezeya, na upepo ikaenda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Angani ilipo'ngiya, eneole ikatanda
Uzi nikaachiliya, 'kadhani itajipinda
Nyuma kuifatiliya, tiara 'kazidi kwenda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Wapi imepoteleya, tiara niliyopenda?
Vipi nitaifikiya, na kupaa kwanishinda?
Ni hofu kuvumiliya, na jinsi nilivyokonda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Mlo nazo 'sinambiya, nimeapa kutopenda!
Tiara zina kayaya, kupozi nazo kwa inda!
H'wenda ikawa kinaya, dhidi ya pepo 'zilinda!
Kukosa ulichopenda, rahisi kukichukiya!
Ahsante sana hewala, kwa auni za busara!
Nilikuwa nimelala, nikiwaza kwa hasira
Bali nasema Inshalla! Nitaipata tijara!
Nilomsifu "Tiara", kwangu ameshakugura!
Pishi nashindwa kulila, pendo halina sitara
Chumba tulopamba sala, nakiona ja ahera
Mola ukiwa ni hila, nipe mwengine kisura!
Nilomsifu "Tiara", kwangu ameshakugura!
Nimelingana kwa Mola, atujeze maghufira
Apate alo aula, nami nimpate bora
Mambo yasiwe ghafula, huvuta heri subira!
Nilomsifu "Tiara", kwangu ameshakugura!
DIWANI YA MRATIBU, 2013.
HII KENYA, KENYA GANI?
Nina hasira moyoni, nimeshindwa vumiliya!
Namsaili Manani, satuwa kusubiriya
Visa tuliona Pwani, kamwe visijerudiya!
Mbwa-mtu tangu lini, "mapenzi" kuyadoweya?
Kaja huyo Baniani, mapeni kuwapatiya
Na kamera mkononi, mbwa kamfunguliya!
Mabinti zetu jamani, mbona soni mwajitiya?
Mbwa-mtu tangu lini, "mahaba" kuyatezeya?
'Wapenzi' niambiyani, nisije potoka njiya
Mbona tumejilaani, kwa nyendo zilopoteya?
Hii sasa Kenya gani, mahoka twajitupiya?
Mbwa-mtu tangu lini, "ngono" wakafurahiya?
Nema mbiu napigani, naomba mnisikiya!
Mili yetu ya thamani, maradhi jiepushiya!
Mabinti nanyi mabini, rekebisheni tabiya!
Mbwa-mtu tangu lini, kitanda kujilaliya?
Nimefurahi wendani, kwa hili kulitangiya
Sote tukaunganeni, tuipige vita haya!
'Tendo la uhayawani, unajisi latutiya:
Mbwa-mtu tangu lini, nikaha kushirikiya?
Glen umebusuri, ni bora huyo wa Nyeri
Mie naona ni heri, ameikata dhakari!
Kilema uwe vizuri, mzima uchomwe nari!
Mbwa-mtu tangu lini, sahani moja kuliya?
Namunukuu Karima, kwa neno la Bibliya:
"Ni bora uwe kilema, mbinguni ukaingiya
Kuliko kuwa mzima, Jehannum kupoteya!"
Mbwa-mtu tangu lini, kudongozaniya njiya?
Namsaili Manani, satuwa kusubiriya
Visa tuliona Pwani, kamwe visijerudiya!
Mbwa-mtu tangu lini, "mapenzi" kuyadoweya?
Kaja huyo Baniani, mapeni kuwapatiya
Na kamera mkononi, mbwa kamfunguliya!
Mabinti zetu jamani, mbona soni mwajitiya?
Mbwa-mtu tangu lini, "mahaba" kuyatezeya?
'Wapenzi' niambiyani, nisije potoka njiya
Mbona tumejilaani, kwa nyendo zilopoteya?
Hii sasa Kenya gani, mahoka twajitupiya?
Mbwa-mtu tangu lini, "ngono" wakafurahiya?
Nema mbiu napigani, naomba mnisikiya!
Mili yetu ya thamani, maradhi jiepushiya!
Mabinti nanyi mabini, rekebisheni tabiya!
Mbwa-mtu tangu lini, kitanda kujilaliya?
Nimefurahi wendani, kwa hili kulitangiya
Sote tukaunganeni, tuipige vita haya!
'Tendo la uhayawani, unajisi latutiya:
Mbwa-mtu tangu lini, nikaha kushirikiya?
Glen umebusuri, ni bora huyo wa Nyeri
Mie naona ni heri, ameikata dhakari!
Kilema uwe vizuri, mzima uchomwe nari!
Mbwa-mtu tangu lini, sahani moja kuliya?
Namunukuu Karima, kwa neno la Bibliya:
"Ni bora uwe kilema, mbinguni ukaingiya
Kuliko kuwa mzima, Jehannum kupoteya!"
Mbwa-mtu tangu lini, kudongozaniya njiya?
MKAMIA MAJI
Ni kipi kinokuliza, mayowe twayasikia?
Walia kufululiza, 'kitweta kila hatua!
Huwajali watuliza, sikio 'mewazibia!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
Mtu akikutuliza, uwache kumfokea
Bila ya kumfukuza, ni vema kumsikia!
Ujapokosa nyamaza, wacha tishiatishia!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
Ndugu epuka matata, nakupa huu wosia
Kwa udi kutotafuta, makuu kujitakia
Unajigamba u jeta, utu umeshauvua!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
Waparamia mafuta, ki ki ki washikilia
Jaala hutoifuta, aloandika Jalia!
Mpiga ngumi ukuta, makono yataumia!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
(DIWANI YA "MRATIBU", 2013).
Walia kufululiza, 'kitweta kila hatua!
Huwajali watuliza, sikio 'mewazibia!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
Mtu akikutuliza, uwache kumfokea
Bila ya kumfukuza, ni vema kumsikia!
Ujapokosa nyamaza, wacha tishiatishia!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
Ndugu epuka matata, nakupa huu wosia
Kwa udi kutotafuta, makuu kujitakia
Unajigamba u jeta, utu umeshauvua!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
Waparamia mafuta, ki ki ki washikilia
Jaala hutoifuta, aloandika Jalia!
Mpiga ngumi ukuta, makono yataumia!
Uwache kukililia, usichoweza kupata!
(DIWANI YA "MRATIBU", 2013).
Jumamosi, 10 Agosti 2013
ASIYEKULA N'NANI?
Nani asiye na meno, asojuwa kutafuna?
Avitikise viuno, hadharani tumuwona!
Miguu na visigino, na njaa asopambana!
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
Us'o hata moya yino, mdomo uloshikana!
Usiye na mzozano, uchu wala tumbo huna!
Mbeleni pa makutano, kashangaze hadhirina!
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
Kinywato tenye mshono, kizibwato kisinena
Kwao uzi na sindano, tito kimeshikamana
Wata mbwende za maneno, vitendo mmekazana
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
Wengi wana mapambano, maghala kujalizana
Mahindi njugu na ngano, kusudi kushibishana
Kuku utafu mdono, wapitapo tunanuna!
Mavi usoyala mbona nawe kuku wawawinga?
Nimekoma beti tano, tuwate kususiana
Hata wawe konokono, ni viumbe vya Rabana
Ujapovila vinono, mwenzio simtukana!
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
(DIWANI YA "MRATIBU", 2013)
Avitikise viuno, hadharani tumuwona!
Miguu na visigino, na njaa asopambana!
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
Us'o hata moya yino, mdomo uloshikana!
Usiye na mzozano, uchu wala tumbo huna!
Mbeleni pa makutano, kashangaze hadhirina!
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
Kinywato tenye mshono, kizibwato kisinena
Kwao uzi na sindano, tito kimeshikamana
Wata mbwende za maneno, vitendo mmekazana
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
Wengi wana mapambano, maghala kujalizana
Mahindi njugu na ngano, kusudi kushibishana
Kuku utafu mdono, wapitapo tunanuna!
Mavi usoyala mbona nawe kuku wawawinga?
Nimekoma beti tano, tuwate kususiana
Hata wawe konokono, ni viumbe vya Rabana
Ujapovila vinono, mwenzio simtukana!
Mavi usoyala mbona, nawe kuku wawawinga?
(DIWANI YA "MRATIBU", 2013)
Ijumaa, 9 Agosti 2013
VUTA HATUWA
Uje nikakuzawiji, nyumbani uwe siraji
Ndivyo ninavyotaraji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
Uwe ukinipa maji, unipikie na uji
Kila ninapohitaji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
Moyoni unifariji, uwe wangu mnoaji
Regina wangu mbuji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
Ndoa yetu tudariji, ijapo sina mitaji
Mwenyezi ndiye Mpaji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
(Kwa Huba Langu Laazizi, Regina Wango Muthelya, 2013).
Ndivyo ninavyotaraji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
Uwe ukinipa maji, unipikie na uji
Kila ninapohitaji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
Moyoni unifariji, uwe wangu mnoaji
Regina wangu mbuji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
Ndoa yetu tudariji, ijapo sina mitaji
Mwenyezi ndiye Mpaji,
Mpenzi,
Vuta hatuwa!
(Kwa Huba Langu Laazizi, Regina Wango Muthelya, 2013).
Jumapili, 4 Agosti 2013
ZIMWI
Linalokujuwa zimwi, ukakwisha halikuli
Kiu chake hakizimwi, kwa utamu wa asali!
Ada kwake haisomwi, majirani huwajali
Matajiri mashendea, upatapo wanalia!
Wakamsimanga tembo, na ukubwake wa kimo
Wajapotowa minyambo, mto chura sende mumo
Silaha sio misimbo, fanza mambo kwa kipimo
Mkongani kaingia, mwisho tembo lililia!
Wa sitara hasumbuki, japokosa maakuli
Asumbuka mwenze chuki, wa moja havai mbili
Juwa baada ya dhiki, na faraja huwasili
Shetani hunyong'onyea, goti Mola kipigia!
Kiu chake hakizimwi, kwa utamu wa asali!
Ada kwake haisomwi, majirani huwajali
Matajiri mashendea, upatapo wanalia!
Wakamsimanga tembo, na ukubwake wa kimo
Wajapotowa minyambo, mto chura sende mumo
Silaha sio misimbo, fanza mambo kwa kipimo
Mkongani kaingia, mwisho tembo lililia!
Wa sitara hasumbuki, japokosa maakuli
Asumbuka mwenze chuki, wa moja havai mbili
Juwa baada ya dhiki, na faraja huwasili
Shetani hunyong'onyea, goti Mola kipigia!
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)